Kutokana na wilaya ya Makete kuwa miongoni mwa wilaya chache hapa nchini kuzalisha kwa wingi matunda aina ya matofaa maarufu kama apples, halmashauri ya wilaya ya Makete imeamua kushirikiana na wadau kupanua wigo wa kilimo hicho ili kizidi kuleta tija kwa wakulima
Hayo yamebainika kufuatia kampuni ya TAHA yenye makao yake jijini Arusha ambayo inahusika na uboreshaji wa mazao ya bustani kufika wilayani Makete na kujadiliana kwa pamoja na halmashauri hiyo na kuweka mikakati ambayo itasaidia kushirikiana kwa pamoja kuboresha kwa kiasi kikubwa kilimo cha matofaa(apples)
Akizungumza na mtandao huu hivi karibuni, Bwana Shamba wa TAHA Bw. Manfred Mitala amesema wiaya ya Makete imekuwa ikifanya jitihada nyingi za kuinua kilimo hicho hivyo ujio wao utasaidia kuboresha na kuongeza nguvu za pamoja katika kuboresha kilimo hicho
Hayo yamebainika kufuatia kampuni ya TAHA yenye makao yake jijini Arusha ambayo inahusika na uboreshaji wa mazao ya bustani kufika wilayani Makete na kujadiliana kwa pamoja na halmashauri hiyo na kuweka mikakati ambayo itasaidia kushirikiana kwa pamoja kuboresha kwa kiasi kikubwa kilimo cha matofaa(apples)
Akizungumza na mtandao huu hivi karibuni, Bwana Shamba wa TAHA Bw. Manfred Mitala amesema wiaya ya Makete imekuwa ikifanya jitihada nyingi za kuinua kilimo hicho hivyo ujio wao utasaidia kuboresha na kuongeza nguvu za pamoja katika kuboresha kilimo hicho
Bw. Mitala amesema mwaka jana rais Kikwete alipofanya ziara wilayani Makete alifurahishwa na taarifa iliyotolewa na halmashauri kuwa kilimo cha apple kinapatikana pia wilayani hapo, hivy aliagiza kilimo hicho kiboreshwe zaidi kwa kushirikiana na wataalamu mbalimbali, na ndiyo maana halmashauri hiyo imeanza kutekeleza agizo hilo kwa kushirikiana na shirika lake
Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Makete mh. Daniel Okoka amesema kwa kuanzia shirika hilo litafanya kazi kwenye kata 12 za wilaya ya Makete ikiwemo kata ya Iniho na kuongeza kuwa kata nyingine ambazo watafanya nazo kazi zitatangazwa hivi karibuni pindi utekelezaji utakapo anza
Mh. Okoka amesema hadi kufikia mwaka 2015/2016 wilaya imejiwekea lengo la kuwa na miche 120,000/= ya matofaa (apples) na jitihada za pamoja zitasaidia kufikia lengo hilo la halmashauri kupiga hatua katika sekta ya kilimo
Mh. Okoka amesema hadi kufikia mwaka 2015/2016 wilaya imejiwekea lengo la kuwa na miche 120,000/= ya matofaa (apples) na jitihada za pamoja zitasaidia kufikia lengo hilo la halmashauri kupiga hatua katika sekta ya kilimo