AFISA ELIMU SEKONDARI WILAYA YA MAKETE ATOA UFAFANUZI KUHUSU USAJILI WA SEKONDARI YA ISAPULANO

Wananchi wametakiwa kutambua kuwa usajili wa shule ya sekondari si hatua rahisi inayoweza kufanywa mara moja, na badala yake watambue kuwa ni mchakato mrefu wenye hatua kadhaa ambazo lazima kila moja ipitiwe kikamilifu ndiyo usajili upatikane

Ufafanuzi huo umetolewa na Afisa elimu sekondari wilaya ya Makete Mwl. Jacob Meena wakati akizungumza na mtandao huu uliotaka kufahamu sababu za kutokamilika kwa usajili ya sekondari ya kata ya Isapulano kama ambavyo imekuwa ikilalamikiwa na wakazi wa kata hiyo

Mwl. Meena amesema ni kweli mchakato wa kuisajili shule hiyo unaendelea hivyo wananchi wanapashwa kuwa na subira kwa kuwa hatua za usajili zinafuatwa ngazi kwa ngazi na wakati mwingine huchukua muda mrefu hivyo wananchi wasione kama suala hilo limepuuzwa bali linaendelea kufanyiwa kazi hadi hivi sasa

Amesema tayari walishafika wakaguzi kuikagua shule hiyo na kutoa mapendekezo ambayo yanatakiwa kukalimishwa ikiwemo suala la ujenzi wa maabara kwani ni agizo lililotolewa na rais Jakaya Kikwete kuwa shule zote za sekondari nchini lazima ziwe na maabara ifikapo Novemba mwaka huu

Ameongeza kuwa hicho ni kigezo kimojawapo ambacho wakaguzi hao watakapouja tena mwezi ujao kuja kuikagua shule hiyo na kukuta haina maabara hawawezi kutoa usajili hivyo kuwaomba wananchi kushirikiana kwa pamoja kuhakikisha shule hiyo inakuwa na maabara


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo