WANAFUNZI 292 KYELA HAWAJAJIUNGA NA MASOMO,WENGI WAPATA UJAUZITO.

Na Ibrahim Yassin,Kyela

WANAFUNZI 292 waliochaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha kwanza wilayani Kyela mkoani Mbeya hawajaripoti shuleni kuanza masomo kutokana na matatizo mbalimbali zikiwamo ya kupata ujauzito kwa wanafunzi wa kike.

Kauli hiyo ilitolewa jana na mkuu wa Wilaya hiyo Magret Malenga wakati akipokea msaada wa vitanda 20 vyenye thamani ya million tatu vilivyotolewa na kampuni inayojishughurisha na ununuzi wa zao la kakao ya Olam Tanzania Limited kwa ajili ya bweni la wanafunzi wa kike katika shule ya Sekondari ya kata ya Busale iliyopo Stamiko Kiwira Cor mine (KCM).

Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa mwaka jana wanafunzi hao hawakuripoti kuanza masomo na wao kama Serikali watafanya msako wa nyumba hadi nyumba ili kuwabaini waliosababisha wanafunzi hao wasiripoti shuleni ikiwemo ya kuwachukulia hatua wale waliowapa ujuzito watoto hao kwa lengo la kuthibiti hali hiyo isitokee tena.

Aliongeza kuwa wilaya ya Kyela bado inachangamoto kubwa katika ufauru kwa wanafunzi na kuwa kwa kuliona hilo Serikali kwa kushirikiana na waau wameamua kujenga mabweni ili kuwapa urahisi wanafunzi kuweza kusoma kwa ufanisi zaidi na kupunguza vishawishi wanavyovipata mitaani.

Diwani wa kata hiyo Ezekia Msyani mbali na kuipongeza kampuni hiyo kwa kuwapatia msaada huo pia aliwataka viongozi wa bodi kuitisha kikao cha pamoja na wazazi wa anafunzi ili kupanga namna ya kuweza kukamirisha taratibu na namna ya kuwawezesha wanafunzi hao kuanza kulala kwenye bweni hilo na kuwa ifikapo tarehe 30 mwezi wa pili watoto wawe wameanza kulala katika bweni hilo.

Mkuu wa shule hiyo Juma Kaniki alisema yeye kwa kushirikiana na waalimu wenzake watahakikisha wanawalinda wanafunzi hao ili wazingatie masomo yatakayopelekea kuongeza ufaulu na kuwa wanafunzi watapata chakula cha mchana na gharama za hostel ni 30,000 kwa mwaka na 120 000 kwa ajili ya chakula na hivi sasa wanajenga uzio ili kudhibit utolo kwa wanafunzi hao.

Mch,Benedictor Mwansasu mkazi wa kijiji hicho aliitaja changamoto inayopelekea wanafunzi wa kike kuolewa na wakiume kujishughurisha na vibarua huku wakiacha shule ni kutokana na waalimu  wa shule hiyo kupenda kuwachapa viboko mara kwa mara wanafunzi hao ambao uamua kuacha shule na kujiingiza katika vitendo hivyo ambavyo vinachangia kushusha elimu wilayani hapa.

Akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wenzake Gedtrida Fabian alisema kuwa kitendo cha kampuni hiyo kuwapatia msaada huo wa vitanda utawapa hueni ya kupata vishawishi mitaani na kuwa watajikita na kusoma kwa bidii ili kuifanya kampuni hiyo ipate nguvu tena ya kuweza kuwasaidia pindi watakapohitaji msaada mungine.

Meneja wa kampuni hiyo Godfrey Okungu kwa upande wake alisema kampuni hiyo imetoa sehemu ya faida inayoipata katika kuuza zao hilo kusaidia vitanda hivyo kwa lengo la  kupunguza changamoto zilizopo mashuleni na kuwa wataendelea kusaidia pale watakapo ombwa kufanya hivyo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo