MWANAUME ALIYEDAIWA KUFARIKI "AMEFUFUKA" NA KISHA KUFARIKI TENA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjCfulFNhbMEBh0lZTwq3XwZD1tg45kZuDoqpd4iqi5LouXBTGutU6VRv1k7rCl_UVHS7OsZegIQjIJnjRz8FGTDCm1AFZipPWLIqCK77u2yYRNyxfcXZKXT982IOw4qdsBcCNpeB976Ow/s1600/kaburi.jpg 
MARAFIKI wa mwanamume ambaye alikuwa amedaiwa kufariki walipigwa na butwaa na kutoroka baada ya mwanamume huyo kugunduliwa kuwa alikuwa hai katika ufuo wa Machakos Level Five leo adhuhuri.
Polisi walikuwa wamepata mwili wa mchuuzi huyo anayedaiwa kuwa wa umri wa miaka 45 katika mtaro kwenye kituo cha mabasi cha Machakos. 

Walifululiza hadi kwenye mochari wakiandamana na marafiki zake lakini wahudumu walipouchunguza ‘mwili’ wakagundua kwamba mchuuzi huyo alikuwa anapumua.

Wahudumu hao walimkimbiza hadi kwenye wodi iliyo karibu na akawekwa mirefeji ya kupumua, kupewa dawa na kuongezwa maji mwilini. Madaktari walisema alikuwa amedhoofika kiasi kwamba hangeweza kupata tena fahamu. Baadaye alifariki mwendo wa saa nane.

Marafiki zake walijawa na huzuni mwili wa mchuuzi huyo ulipokuwa ukipelekwa kwenye mochari mara ya pili. Jina la mwanamume huyo halikutolewa, huku madaktari wakisema wanasubiri jamaa zake wafahamishwe rasmi kuhusu kifo chake.

Marafiki zake waliohojiwa na KNA walisema marehemu alipokuwa hai alikuwa amelalamika kwamba alikuwa anahisi maumivu makali kifuani. Walisema mchuuzi huyo alikuwa ameonywa dhidi ya kunywa pombe kupindukia kwa sababu alikuwa na matatizo ya kiafya.

Walisema alikuwa amelala mtaroni kwa zaidi ya masaa sita baada ya kunywa pombe.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo