MAWASILIANO YA BARABARA YA MAKETE-BULONGWA-MBEYA HATARINI KUKATIKA KUTOKANA NA MVUA

Kufuatia kuwepo hatari ya kukatika mawasiliano ya barabara ya Makete-Bulongwa-Mbeya kufuatia kumeguka kwa kingo za barabara karibu na daraja la Ilolo wilayani Makete mkoani Njombe kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha wilayani hapo, wahusika wametakiwa kulichukulia uzito suala hilo

Mtandao huu umeshuhudia hatari ya kumeguka kwa barabara katika eneo hilo hali ambayo endapo haitachukuliwa hatua za haraka itasababisha barabara hiyo kukatika na kutopitika kabisa

Kufuatia hatari hiyo, mwandishi wa mtandao huu alibisha hodi ofisini kwa mkuu wa wilaya ya Makete mh Josephine Matiro ambaye alikiri kupata taarifa za tukio hilo ambapo aliwasiliana kwa njia ya simu na meneja wa TANROADS mkoa wa Njombe ambao waliahidi kufika mara moja kwenye eneo hilo

Mh. Matiro amesema anatambua adha ambayo wakazi wa makete wataipata endapo eneo hilo litakatika na kuahidi kuendelea kulisimamia ipasavyo suala hilo hadi litakapomalizika ili kuondoa usumbufu utakaojitokeza

Mwandishi wa mtandao huu amefika eneo hilo na kukuta hatua za awali zilizochukuliwa na TANROADS mkoa wa Njombe ambao kama walivyosema watafika mara moja ni kweli walifika na kuzungushia alama za tahadhari eneo hilo huku wakiendelea na hatua zaidi za kukarabati eneo hilo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo