MISS Tanzania 2004, Faraja Kota
amefunguka kuwa kamwe hawezi kuingilia kazi za mumewe ambaye ni Waziri
wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu kwani anaamini mumewe ana akili
nyingi kuliko yeye.
Akizungumza na paparazi wetu, Faraja
alisema siyo rahisi kuingilia kazi za mume wake zaidi ya kuzungumza naye
kidogo sana kama kuna kitu amekiona anaweza kumshauri kwa sehemu fulani
lakini siyo kwa kiasi kikubwa sana.
Faraja Kota.
“Unajua mume wangu ana akili zaidi
kuliko hata mimi, naweza kumshauri kidogo tu kama nitakiona kitu fulani
na siyo vyote kwa sababu ninaporudi nyumbani anakuwa ni baba zaidi na
siyo kama waziri,” alisema Faraja.