TANZANIA
imezidi kupaa kwenye viwango vya ubora wa Shirikisho la Soka la
Kimataifa (FIFA) baada ya kupanda kwa nafasi nne na sasa ni ya 120
kutoka nafasi ya 124 mwezi uliopita.
Viwango hivyo vimetoka ikiwa ni takribani wiki moja kupita tangu Tanzania itoke kwenye michuano ya Kombe la Chalenji inayoandaliwa na Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA)
