WATOTO WATATU WAFARIKI DUNIA BAADA YA KUFUKIWA NA KIFUSI WILAYANI KISARAWE

Watoto watatu wenye umri kati ya miezi mitano na miaka 13 wakazi wa kitongoji cha Kibong'wa wilayani Kisarawe wamekufa papohapo baada ya kufunikwa na kifusi cha udongo.
 
Watoto hao walifunikwa na kifusi hicho baada ya wazazi wao kuwaweka katika eneo lililochimbwa kifusi awali ili wajikinge na jua huku wao wakiendelea na kazi hiyo na ndipo ghafla kilipodondoka kifusi kwenye eneo walilokuwepo watoto hao.

Mganga wa zamu kwenye hospitali ya wilaya Kisarawe Dkt, Hamza Mzige amethibitisha kupokea maiti za watoto hao Asnat Semeni(miezi mitano),Twaha Ally (2)na Mwazani Salehe(13),ambapo amesema vifo vyao vimetokana na Kukosa hewa baada ya kufunikwa na kifusi hicho.

Majeruhi amina amiri ambaye hadi sasa hajafahamu kupoteza maisha mtoto wake twaha allyaliyelazwa wodi namba nne hsopitalini hapo amesema alikuwa amewaweka watoto hao ilikujikinga na jua ghafla aliposikia kishindo na kuomba msaada.

Mkuu wa wilaya Kisarawe Fatuma Kimario aliyefika hospitalini hapo amesema machimbo hayo ya Muilembe serikali ilipiga marufuku na kubandika mabango ya kukataza  na watu wamekuwa wakijiiba kwenda kuchimba kokoto.

Itv iliyokuwepo katika eneo hilo ilishudhudia kuwepo ukimya mkubwa baada ya wachimbaji wengi kukimbia eneo hilo wakiogopa kukamatwa na kuacha vifaa vyao vya kazi.

Chanzo:ITV


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo