VIGOGO WA SERIKALI WILAYANI ROMBO WAIBWAGA TAKUKURU MAHAKAMANI

Mahakama ya Wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro, imewaachia huru vigogo watano wa halmashauri ya wilaya hiyo, waliokuwa wakikabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi.
 
Kesi hiyo ilifunguliwa Juni 13 mwaka huu na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) iliyokuwa ikiwatuhumu vigogo hao kuisababishia halmashauri hasara ya Sh29.9 milioni.
Hukumu ya kuwaachia huru washtakiwa hao waliokuwa wakitetewa na wakili Duncan Oola wa jijini Arusha, ilitolewa Ijumaa iliyopita na Hakimu wa Wilaya ya Rombo, Yohana Myombo.
Walioachiwa huru na nyadhifa zao zikiwa kwenye mabano ni Joseph Ngoseki (Ofisa Elimu), Emmanuel Masele (Mweka Hazina) na Elias Mshana, (Kaimu Mkurugenzi).
Wengine ni Erick Barongo (Mhasibu) na Rahel Mshangila (Ofisa Ugavi Msaidizi.
Katika hukumu yake, Hakimu Myombo alisema upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha mashtaka hayo.
Juni mwaka jana, Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Maghella Ndimbo, alidai kuwa makosa yalitendeka Septemba  mwaka  2007.

Na Daniel Mjema, Mwananchi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo