TATIZO LA NGUZO ZA UMEME KUANGUKA BARABARA YA ALI HASSAN MWINYI, TANESCO YATOLEA UFAFANUZI

Kufuatia tatizo la kugongwa na kuanguka kwa nguzo za msongo mkubwa zaidi ya tano katika Barabara ya Ali Hassan Mwinyi, Afisa Uhusiano wa Tanesco, Badra Masoud amefunguka na kusema kuwa mafundi wapo kazini ambapo umeme utarejea kuanzia saa 1:00 usiku.
 
Akizungumza na mtandao huu muda mfupi uliopita, Badra alisema hadi muda huu polisi hawajanikiwa kuwakamata wahusika waliogonga nguzo moja na kusababisha nyingine kuanguka usiku wa kuamkia leo.

"Tatizo ni kubwa lakini mafundi wetu wapo kazini. tunatarajia hadi ifikapo saa moja usiku umeme utawaka maeneo yote yaliyoathirika hasa Kijitonyama," alisema Badra akiliomba jeshi la polisi kuwakamata haraka wahusika wa tatizo hilo.

Usiku wa kuamkia leo dereva asiyejulikana aligonga nguzo moja ya umeme jirani na Chuo Cha Posta Kijitonyama iliyoangusha nguzo zingine tano na kusababisha mlipuko mkubwa wa moto katika Barabara ya Ali Hassa Mwinyi maeneo ya Bamaga.

CREDITS:GPL


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo