Gazeti la The Star la Kenya liliandika kuwa staa huyo alitapeli advance ya show mbili za Kenya na kumfanya promota wa show hizo afungue kesi mjini Mombasa na kumuita Mr Blue ni tapeli na kwamba anatafutwa na polisi.
Mr Blue amesema promota huyo aliwasiliana na Mr Blue fake na wakakubaliana kuhusu show hizo lakini baadaye akawa ameingia mitini.
"Mwisho wa siku kumbe sio mimi. Jamaa amekuja kunipigia simu ananilalamikia nikamwambia 'mimi sijui chochote, kwanza sipo kwenye Facebook'", amesema Kabayser. Amesema hakuwa na kitu cha kumsaidia promota huyo kwakuwa alikuwa tayari na show zingine hapa nchini na hivyo asingeweza kuokoa jahazi.
Sikiliza sauti yake hapa akizungumza na redio citizen ya Kenya(credits:bongo 5)