Mwigizaji, muongozaji wa filamu na mmiliki wa
kampuni wa filamu ya 5effects William Mtitu amepata bahati ya kuongeza
idadi ya wanafamilia wake baada ya mke wake Jovitha Mtitu kujifungua
salama mtoto wao wa kwanza kwenye hospitali ya Regency jijini Dar es
salaam hivi majuzi.
Kupitia ukurasa wa mtandao mmoja wa kijamii Mtitu aliandika…
“Nawashukuru madaktari wa hospital ya regency na kwa Dr mvungi
wakiongozwa na Dr getu kwa kusaidia mpaka mke wangu kujifungua salama na
sasa naitwa baba na mke wangu mama ,kwa kweli mungu awabaliki sana…”
Hali ya Mama na mtoto ni njema na wanaendelea vizuri. Hongera sana Mtitu na familia yako.