Gazeti la raia mwema limeagizwa kumuomba radhi mbunge wa Kinondoni jijini DSM Iddi Azan kwa kuandika habari za uongo dhidi yake kuwa anajishughulisha na biashara ya dawa za kulevya
Pamoja na hayo pia gazeti hilo limetakiwa kumuita Iddi Azana na kufanya naye mahojiano ya kina kwa namna alivyohusishwa na suala hilo, pamoja na kumlipa gharama zote za mwenendo wa shauri hilo hadi maamuzi hayo yakatoka
Maamuzi hayo yametolewa na baraza la habari Tanzania MCT, kufuatia malalamiko yaliyotolewa na mbunge huyo kuwa hakutendewa haki na gazeti hilo
Mbunge Azan amesema kwa yeye anashukuru sana kwa kuwa licha ya suala hilo kumuathiri, lakini wananchi wake walizidi kumpa ushirikiano kama kawaida huku wengine wakimuombea dua