 |
| Nyumba iliyoingiliwa na maji hadi ndani |
Ikiwa
ndio mvua za awali za masika zimeanza kunyesha katika mikoa ya Kanda ya ziwa,
huenda katika siku zijazo zikaleta madhara makubwa kutokana na tatizo la
miundombinu hasa katika wilaya ya kahama.
Hii
inafuatia mvua iliyonyesha leo kwa muda wa saa moja tu katika mji wa kahama na
kujaza maji katika baadhi ya nyumba za wananchi, nyumba za kulala wageni na
hata katika nyumba za maduka ya biashara hasa katika mitaa ya majengo na
Nyasubi mjini humo.
 |
| Nyumba nyingine ambayo pia maji yamejaa ndani |
Katika
muda wa takriban saa moja na nusu magari, pikipiki, baiskel na hata watembea
kwa miguu walisimama kutokana na kushindwa kuvuka katika maji yaliyojaa katika
kalvati na kutapika juu ya barabara.
Endelea
kuangalia matukio katika picha hapa…
 |
| Ilikuwa ni balaa tupu |
 |
| Mfanyabiashara akijaribu kuzibua kalvati liloziba ili maji yatoke katika eneo lake |
 |
| Maji yanavyotapika juu ya kalvati, tena hapa yamepungua |
 |
| Maji yalivyojaa barabarani duhhh!! |
 |
| Kila mmoja natafuta pa kupita |
 |
| Mitaa hii hakufai |
 |
| Kupita kwa miguu tatu, Bodaboda tabu |
 |
| Baadhi ya Familia wakishangaa hali ilivyo |
 |
| Duhh! Barabara haitamaniki |
 |
| Sijui gari zitapitaje wakati masika inaendelea |
Kiukweli katika hili serikali inatakiwa kuboresha sana Miundfombinu hasa ya Barabara katika mji huu wa madini Kahama!!
Chanzo: Faraji Mfinanga via DUNIA KIGANJANI BLOG
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi