AFRIKA KUSINI YASITISHA UOKOAJI KWA MUDA....!!!!!


 

Jitihada za uokoaji zimesitishwa kwa muda baada ya paa la jengo la maduka lililokuwa linajengwa kuporomoka nchini Afrika Kusini.

Msemaji wa Polisi Thulani Zwane ameiambia BBC kwamba kazi ya kuwatafuta watu walionusurika itaanza tena baada ya kuondoa baadhi ya matofali.
Mtu mmoja ameripotiwa kufa na wengine 40, wengi wao wakiwa ni mafundi wa ujenzi wanahofiwa kukwama katika kifusi katika eneo la ujenzi la Tongaat, kaskazini mwa Durban.
 
Watu wapatao 30 wameokolewa, baadhi yao wakiwa katika hali ya taharuki.

Kepteni Zwane amesema watu 11 miongoni mwa waliopelekwa hospitali wamejeruhiwa vibaya.

Naibu meya wa mji wa Tongaat ameviambia vyombo vya habari vya Afrika Kusini kuwa serikali ilipata amri ya mahakama mwezi mmoja uliopita, kusitisha ujenzi katika eneo la Tongaat, ambao ni mji mdogo uliopo kilomita 40 kaskazini mwa Durban.

BBC


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo