RAIS KIKWETE AWA MGENI RASMI KATIKA JUBILEI YA MIAKA 100 YA PAROKIA YA LUGOBA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo Jumapili, Oktoba 27, 2013 akiwa na Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki  wa Jimbo la Morogoro Onesphory  Mkude, Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Tanga Anthony Banzi, Viongozi wa mkoa wa Pwani, Kamati ya Walei ya Parokia ya Lugoba wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani, Waumini na Wananchi, amehudhuria kwenye sherehe za Jubilei ya kuadhimisha Miaka 100 ya Parokia hiyo.  Zifuatazo ni baadhi ya picha kutoka kutoka Ikulu kuhusu tukio hilo.
Rais Kikwete akiwaonesha Askofu Mkude, Askofu Banzi na viongozi wa mkoa wa Pwani iliyokuwa inaendeshwa na darasa alilosomea wakati alipokuwa Shule ya Kati ilinayoendeshwa na Parokia ya Lugoba
Rais Jakaya Kikwete akikata utepe kuzindua zahanati katika Parokia ya Lugoba
Rais Kikwete na Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki wa Jimbo la Morogoro Onesphory Mkude, wakishuhudiwa na Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Tanga Anthony Banzi, wakiweka jiwe la msingi
Rais Kikwete akiwa na Askofu Mkude, Askofu Banzi, viongozi wa mkoa wa Pwani na Kamati ya Walei ya Parokia ya Lugoba.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo