Jumla ya
Wanafunzi 84 wanatarajia Kufanya Mitihani yao ya Kuhitimu Darasa la
Saba Katika shule ya Msingi ya St.Benedict Iliyoko Ramadhani Mjini
Njombe.
=============
Adha ya Maji Katika Mkoa wa Njombe Imetajwa Kuwa Kikwazo hadi kwenye Sekta ya Elimu Kutokana na Wanafunzi wengi Kutumia Muda Mwingi Kutafuta Maji Badala ya Masomo
Tatizo Hilo la huduma maji Mkoani Hapa Limeendelea kuwa changa moto kubwa kwa shule nyingi za msingi na sekondari hali inayo pelekea wanafunzi kutumia Muda Mwingi kutafuta maji katika maeneo Ya Mbali na Mazingira ya shule.
Hayo Yamebainishwa na Makamu Mkuu wa Shule ya Mtakatifu Benedict Bw Flaviani Mligo Iliyoko Ramadhani Mjini Njombe wakati wa MaHafali ya 11 ya darasa la saba Agosti 31 Mwaka Huu shuleni hapo ambapo makamu mkuu huyo amesema licha ya shule hiyo kuwa na mabomba lakini Wanalazimika kufuata maji mtoni na visima vya mitaani
Risala ya Wanafunzi Mbele ya Mgeni rasmi Bwana Shejamabu Kutoka Kampuni ya Tanwatt Kibena Imeeleza Kuwa Licha Adha ya Maji na Changamoto Mbalimbali wanazokabliana nazo Lakini watahakikisha wanafanya Vizuri Katika Mitihani yao ya Kuhitimu Darasa la Saba Inayotarajia Kufanyika September 10 na 11 mwezi huu.
Kwa upande wao wazazi wa watoto wanaosoma katika shule hiyo wamewashukuru walimu kwa kuwalea na kuwafundisha huku wakiahidi kuendelea kuwasomesha mpaka elimu ya juu.
Jumla ya Wanafunzi 84 wa Darasa la Saba wanataraji Kufanya Mtihani huo Mwaka Huu Katika Shule Hiyo ya St.Benedict Ambapo Pamoja na Mambo Mengi Uongozi wa Shule Hiyo Umesema Big Results Now Katika Sekta ya Elimu Inahitajika Kuboreshwa Katika Shule zote Bila Kubagua.
=============
Adha ya Maji Katika Mkoa wa Njombe Imetajwa Kuwa Kikwazo hadi kwenye Sekta ya Elimu Kutokana na Wanafunzi wengi Kutumia Muda Mwingi Kutafuta Maji Badala ya Masomo
Tatizo Hilo la huduma maji Mkoani Hapa Limeendelea kuwa changa moto kubwa kwa shule nyingi za msingi na sekondari hali inayo pelekea wanafunzi kutumia Muda Mwingi kutafuta maji katika maeneo Ya Mbali na Mazingira ya shule.
Hayo Yamebainishwa na Makamu Mkuu wa Shule ya Mtakatifu Benedict Bw Flaviani Mligo Iliyoko Ramadhani Mjini Njombe wakati wa MaHafali ya 11 ya darasa la saba Agosti 31 Mwaka Huu shuleni hapo ambapo makamu mkuu huyo amesema licha ya shule hiyo kuwa na mabomba lakini Wanalazimika kufuata maji mtoni na visima vya mitaani
Risala ya Wanafunzi Mbele ya Mgeni rasmi Bwana Shejamabu Kutoka Kampuni ya Tanwatt Kibena Imeeleza Kuwa Licha Adha ya Maji na Changamoto Mbalimbali wanazokabliana nazo Lakini watahakikisha wanafanya Vizuri Katika Mitihani yao ya Kuhitimu Darasa la Saba Inayotarajia Kufanyika September 10 na 11 mwezi huu.
Kwa upande wao wazazi wa watoto wanaosoma katika shule hiyo wamewashukuru walimu kwa kuwalea na kuwafundisha huku wakiahidi kuendelea kuwasomesha mpaka elimu ya juu.
Jumla ya Wanafunzi 84 wa Darasa la Saba wanataraji Kufanya Mtihani huo Mwaka Huu Katika Shule Hiyo ya St.Benedict Ambapo Pamoja na Mambo Mengi Uongozi wa Shule Hiyo Umesema Big Results Now Katika Sekta ya Elimu Inahitajika Kuboreshwa Katika Shule zote Bila Kubagua.
Na Prosper Mfugale Njombe.