MSHTAKIWA ALALAMIKA KUHUSU CHAWA WALIOPO MAHABUSU

Nyeri
Sehemu ya mji wa Nyeri.

MSHUKIWA wa wizi wa mabavu Ijumaa aliomba mahakama ya Nyeri kuharakisha kusikizwa kwa  kesi yake huku akilalamika wingi wa chawa kwa jela haswa wakati wa msimu huu wa baridi.
Hakimu mkuu wa Nyeri, Bi Wilbroda Juma alishtuliwa na madai ya Maina na kumuamuru afisa wa polisi kuhakikisha kuwa ameweza kuchunguza kwa makini madai hayo ya wafungwa kuumizwa na chawa.

Joseph Maina aliomba mahakama iweze kuharakisha kuisikia kesi hiyo kwani anaumia sana akiwa kwenye rumande.

“Imefika miaka miwil sasa na kesi yangu bado haijasikizwa,” aliteta Bw Maina.

Maina ameshtakiwa pamoja na Duncan Mumangari na James Ngunjiri kuwa mnamo siku ya Julai 7, mwaka jana walimuibia Bw James Macharia simu na pesa taslimu zote zikiwa ni za thamana ya Sh14,000 katika kijiji cha Ruring’u katika eneo la Nyeri.

Watatu hao pia wanashtakiwa kumuumiza Bw Macharia kwa kutumia silaha kama vile rungu.

Bi Juma alimhakikishia Maina kuwa mahakama hiyo imeyasikia malalamiko yake na kueleza kuwa kesi imechukua muda mrefu kusikizwa kwani mwendesha wa mashtaka anatafuta uchunguzi kamili kama vile washahidi na ripoti ya daktari kuthibitisha kuwa kwa kweli mlalamishi alikuwa ameumizwa.

“Kesi yenu itasikizwa haraka iwezekanavyo mnamo siku ya Septemba 19,”alieleza Bi Juma.

Kwingineko, mahakama ya Nyeri Ijumaa ilimhukumu mama aliyepatikana na hatia ya kuuza chang’aa.

Esther Wanjiku alipatikana akiuza chang’aa hapo Ijumaa katika kijiji cha Chaka, eneo la Nyeri.

Kiwete
Akijitetea, Wanjiku alisema kuwa amekuwa mgonjwa kwa muda mrefu na anatetemeka kila wakati kwa athari ya dawa anazokunywa za kupunguza makali ya Ukimwi (ARVs).

Wanjiku aliomba mahakama pia imsamehe kwani anamlea mtoto kiwete na watoto wengine watatu.

Hakimu mkuu wa Nyeri, Bi Wilbroda Juma alimueleza mshtakiwa kuwa hawezi msamehe bila kuhukumiwa.

“Mahakama imekupata na hatia na utalipa faini ya Sh30,000 au kifungo cha miezi mbili,”alieleza Bi Juma.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo