MAPOKEZI YA MBIO ZA MWENGE WILAYA YA TEMEKE DSM 2013


Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Bi Sofia Mgema akipokea Mwenge wa Uhuru wilayani mwake.
Baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi za wilaya ya Temeke wakionesha walichokiandaa.
Risala ikisomwa.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke akikabidhi Mwenge kwa Kiongozi wa mbio za Mwenge, Juma Ali SimwaiJuma Ali Simwai (kushoto) akiwa ameketi sehemu aliyoandaliwa, kulia ni wenyeji wake.Mkuu wa Wilaya ya Temeke akikabidhi risala kwa kiongozi wa mbio za Mwenge
Juma Ali Simwai akitoa shukrani zake kwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bi. Sofia Mgema mara baada ya kukabidhiwa risala.

Mbio za Mwenge zilipiga kambi katika Wilaya ya Temeke kwenye Viwanja vya Mbagala Zakhem jijini Dar hapo jana Septemba 6 mwaka huu, ambapo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick na mwenyeji wake Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Bi. Sofia Mgema walihudhuria mapokezi hayo.

Pia viongozi mbalimbali wa serikali, watumishi wa umma na wananchi kutoka sehemu tofauti  hapa jijini Dar kwa pamoja waliupokea Mwenge huo na kushiriki michezo iliyoandaliwa kwa niaba ya kiongozi wa mbio za  Mwenge kwa mwaka huu, Juma Ali Simwai. Kauli mbiu ikiwa ni: 

“Watanzania ni wamoja tusigawanywe kwa misingi ya tofauti zetu za dini, itikadi, rangi na rasilimali.”

(PICHA NA CHANDE ABDALLAH NA DENIS MTIMA/ GPL)


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo