ZAIDI YA WANAFUNZI 300 HAWAJUI KUSOMA WALA KUANDIKA KILA KATA WILAYANI MUFINDI MKOANI IRINGA

Zaidi ya wanafunzi 300 kwa kila kata katika wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, wamebainika kuwa hawajui kusoma, kuandika na kuhesabu kwa mwaka 2012/2013  idadi ambayo imedaiwa kuongezeka mwaka hadi mwaka.
 
Hayo yamebainika katika kikao cha kamati ya ushauri ya Hamashauri ya Wilaya hiyo, ambapo pamoja na suala la wanafunzi kutojua kusoma kuandika na kuhesabu pia kikao hicho kimejadili suala la Mimba mashuleni tatizo ambalo licha ya kupigiwa kelele bado ufumbuzi umekuwa kitendawili.

Wadau wa kikao hicho akiwemo mbunge wa jimbo la Mufindi Kusini Mendrad Kigola,  wametoa maoni mbalimbali  kuhusu tatizo la kutojua kusoma na kuandika, huku upungufu wa vifaa vya kufundishia ukitajwa kuwa ni sababu mojawapo inayosababisha  walimu kushindwa kufundisha  kwa ufanisi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa  halmashauri hiyo, Peter Tweve ametoa maagizo ya jumla kwa watendaji ili kukabilinana na  changamoto ambazo zimeonekana kukwamisha maendeleo ya sekta ya elimu katika Wilaya hiyo.
 
Imedaiwa kuwa wazazi  wengi, wamekuwa wakimaliza kesi  za mimba na watuhumiwa kwa kishawishi cha fedha na kusababisha kesi hizo kutofikishwa katika vyombo vya kisheria.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo