WATU
27 Wameuawa na fisi katika matukio tofuati kwenye mikoa ya Geita na Mwanza
katika kipindi cha mwaka 2012 /2013na wengine saba kujeruhiwa.
Hatua
hiyo imedaiwa kuitisha serkali kutokana na kupotea kwa nguvu kazi kwani wengi
wa wailiouawa ni watoto na tayari Kikosi cha nguvu kazi kimepelekwa kanda ya
ziwa kutoa elimu juu ya tabia ya fisi kwa kutumia sinema na kuwasaka fisi hao.
Katika
taarifa iliyotolewa na Wizara ya Maliasili na Utalii imefafanua kuwa pia fisi
33nao wameuawa na kikosi cha kukabiliana na ujangili kanda ya mwanza
lakini kikwazo kikubwa cha utekelezaji zoezi hilo ni kukosa ushirikiano kutoka
kwa jamii kutokana na kuamini kuwa fisi hao wanafugwa kichawi.
Kikosi
hicho cha nguvu kazi kilichoaza zoezi hilo Agosti 16 mkoani Mwanza kinaongozwa
na Mkuu wa Idara ya Elimu kwa Umma wa Wizara ya Maliasili na Utalii Bwana Twaha
Twaibu akisaidiwa na Bwana Benjamini Kijika Mkuu wa kikosi cha kuzuia ujangiri
kanda ya ziwa.
Katika
utekeelzaji huo wa kutoa elimu kwa jamii katika maeneo yaliyoathiriwa na wimbi
la mauaji ya fisi elimu itatolewa kupitia nadharia na sinema hata hivyo Mkoa wa
Geita ndio ulioathirika zaidi ikilinganishwa na mikoa ya Mwanza na Simiyu na
Shinyanga.
Akizungumzia
hali hiyo mara baada ya kuanza ziara ya kikaziya siku tano Mkoani Geita
juzi Mkuu wa idara ya Elimu kwa Umma wa Wizara ya Maliasili na
utalii Bwana Twaha Twaibu jana amesema kuwa hadi june 2013 familia 93 zilikuwa
zimelipwa kifuta machozi cha shilingi milioni 49 kwa nchi nzima katika matukio
yanayotokana na wanyama wakaliwakiwemo fisi kuua binadamu.
Kwa
mujibu wa sheria wanachi pia wameelezwa kuwa mtu anapouaw a na mnyama familia
yake ina haki ya kulipwa kifuta machozi cha shilingi milioni MOJA,na
aliyejeruhiwa na kuachwa na kilema cha kudumu ni shilingi Lakitatu na
jeraha la kawaida n shilingi Lakimbili na kuachana na imani potofu kuyahusisha
na ushirikina.
Tatizo
la kukabiliana na mauaji yanayofanywa na fisi katika mikoa ya kanda ya
ziwa limekuwana changamoto kubwa kutokana na jamii ..kuyahusisha
matukio hayo na imani za kishirikina na hivyo jamii kutokuwa tayari kutoa
ushirikiano katika kuwasaka na kuwaua fisi wakihofia kudhurika.
