Gavana wa Mombasa Ali Hassan Joho.
Na GALGALO BOCHA na EUNICE MACHUHI.
SHAHIDI aliyejitokeza kutoa ushahidi katika kesi dhidi ya Gavana wa Mombasa, Hassan Joho Jumatatu ya wiki hii alijikuta pabaya alipowekwa rumande kwa kutoa ushahidi potofu licha ya kuapa na kusimama kizimbani.
Bi Zainab
Said alitoa ushahidi kwamba alishuhudia kisa cha utoaji rushwa kwa
wapiga kura katika kituo cha upigaji kura cha Jamvi la Wazee huko
Kisauni.
Kilichomtia
matatani zaidi ni alipoeleza mahakama aliripoti kisa hicho kwa msimamizi
wa kike kituo hapo licha ya stakabadhi za mahakama kuonyesha kwamba
afisa huyo ni mwanamume.
Hata baada ya
Jaji Fred Ochieng kumtaka kutazama stakabadhi ya mahakama iliyoonyesha
wazi afisi huyo ni mwanamume, Bi Said alisisitiza kwamba afisi huyo
alikuwa ni mwanamke.
Jaji Ochieng
aliagiza shahidi huyo kutiwa nguvuni na kuwekwa rumande punde tu
alipoteremka kutoka kizimbani baada ya kutoa ushahidi wake.
“Nina uhahika alikuwa ni mwanamke,” akaeleza Bi Said.
Shahidi
alikuwa ni miongoni mwa mashahidi watatu wa Bw Shahbal waliotoa ushahidi
katika kesi ambapo anataka mahakama ibatilishe uchaguzi wa Bw Joho kama
gavana wa Mombasa.
Ubishi
Jaji Ochieng
alitoa agizo hilo baada ya kutilia shaka ushahidi wa Bi Said ambaye
alikuwa ubishi mwingi kusisitizia mahakama kwamba afisa huyo ni
mwanamke.
Baadaye
Jumatatu jioni Mahakama ilielezwa kwamba tayari polisi wameandika
taarifa kutoka kwake na kupewa agizo la kufika mahakamani baada ya siku
nne.