MTOTO MCHANGA AZIKWA AKIWA HAI MKOANI NJOMBE

ACP Fulgency Ngonyani Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe.

Jeshi la Polisi Mkoani Njombe Linamshikilia Maria Kilasi Ambapo Anatuhumiwa Kutupa Mtoto Mchanga Ndani ya Shimo na Kisha Kumfukia na Kusababisha Kifo cha Mtoto Huyo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe ACP Fulgence Ngonyani Amesema Tukio Hilo Limetokea Agosti 26 Mwaka Huu Majira ya Saa Tano Asubuhi Katika Eneo la Mashujaa Mjini Makambako Baada ya Mbwa Kufukua Mwili wa Mtoto Huyo.

ACP Ngonyani Amesema Mnamo Agosti 23 Mwaka Huu Mtuhumiwa Alijifungua Mtoto wa Kiume na Siku ya Agosti 26 Mwaka Huu Alimfukia Ndani ya Shimo na  Kwamba Upelelezi Dhidi ya Tukio Hilo Linaendelea, Mtuhumiwa Atafikishwa Mahakamani Pindi Upelelezi Huo Utakapokamilika. 

Na Gabriel Kilamlya


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo