Mashamba yaliyopandwa majani chai katika kaunti ya Murang'a. Picha Na SAMUEL KARANJA.
MFANYABIASHARA wa kaunti ya Murang’a aliyetekwa nyara akiwa kaunti jirani ya Kirinyaga amepatikana.
Kulingana na
polisi, Bw Harrison Gichuhi ambaye anamiliki kituo cha mafuta ya petroli
katika soko la Kagio huko Kirinyaga nchini Kenya, alipatikana siku ya Jumanne jioni.
Mfanyibishara huyo alitekwa nyara wiki jana na wakora watatu waliovalia sare za polisi.
“Alitwambia kuwa, alikuwa amefichwa kwenye nyumba moja katika kijiji cha Gikindu kaunti ya Murang’a,” alisema Bw Odede.
Baada ya
kutoroka, mfanyibiashara huyo alipata usaidizi kutoka kwa majirani na
kisha kupelekwa katika kituo cha polisi kuandikisha ripoti.
Watekaji nyara hao walikuwa wameitisha Sh3 milioni ili kumwachilia lakini Bw Odede alisema fedha hizo hazikulipwa.
Hata hivyo,
afisa mmoja wa polisi ambaye aliomba asitajwe jina, aliambia Taifa Leo
kuwa huenda ikawa familia hiyo ililipa watekaji nyara hao kitita fulani
cha pesa.
Bw Gichuhi alishambuliwa na wezi hao mwendo wa saa moja jioni siku ya Alhamisi wiki jana.
Kulingana na
walioshuhudia kisa hicho, walificha gari lao karibu na kituo cha mafuta
na wawili wakatoka nje huku wakitaka kumtia pingu.
Hata hivyo,
alikataa kukamatwa huku akitaka kujua sababu ya kutiwa mbaroni na katika
harakati hiyo, wanaume hao wawili walimtupa ndani ya gari na kutoroka
naye.