MABARAZA YA KATIBA WILAYA YA KIBAHA MKOANI PWANI YAANZA KAZI

1.
Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Prof. Palamagamba Kabudi (wa pili kulia|) akizungumza na Viongozi wa Mkoa wa Pwani leo Ijumaa (Agosti 2. 2013) wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mhe. Halima Kiemba (kushoto), Katibu Tawala wa Mkoa, Bi. Bertha Swai (wa pili kushoto). Wajumbe wa Tume walifika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kupokea  taarifa za maandalizi ya Mikutano ya Mabaraza ya Katiba katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha mkoani humo, kulia ni Mjumbe wa Tume, Mhe. Al-shaymaa Kwegyir.
2.
Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya Katiba, Profesa Palamagamba Kabudi akuizungumza na Wajumbe wa Baraza la Katiba la Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani wakati wa ufunguzi wa mkutano huo uliofanyika leo (Ijumaa Agosti 2, 2013) katika uykumbi wa Shule ya Sekondari ya Kilangalanga iliyopo Wilayani humo.
 3.
Mjumbe wa Baraza la Katiba la Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani, Bi. Fediria Swai akichangia hoja kuhusu Rasimu ya Katiba Mpya iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katika katika mkutano uliofanyika leo( Ijumaa Agosti 3, 2013) katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Kilangalanga iliyopo Wilayani humo.
4.
Mjumbe wa Baraza la Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani, Jenifer Hassani akichangia hoja kuhusu Rasimu ya Katiba Mpya iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika mkutano uliofanyika leo Ijumaa (Agosti 2, 2013) katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Kilangalanga iliyopo Wilayani humo.
5.
Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Profesa Palamagamba Kabudi akizungumza na Wajumbe wa Baraza la Katiba la Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwa ni katika mkutano uliofanyika leo Ijumaa (Agosti 3, 2013) katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Kilangalanga iliyopo Wilayani humo.
6.
Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Profesa Palamagamba Kabudi (kushoto), Al- Shaymaa Kwegyir (katikati) wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Mkoa wa Pwani wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Mhe. Halima Kiemba (wa pili kulia) na Katibu Tawala wa  Mkoa huo, Bi. Bertha Swai mara baada ya Wajumbe wa Tume kupokea taarifa ya Maandalizi ya Mikutano ya Mabaraza ya Katiba katika Halmashauri za Wilaya na Miji ya Kibaha.(PICHA NA TUME YA KATIBA).


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo