KAMPUNI YA HIGHLAND SEED GROWERS YA JIJINI MBEYA YAGAWA MBEGU BORA ZA MAHINDI BURE KWA WAKULIMA MAKETE

 Bwana shamba wa kampuni ya highlands seed growers Iddi Kapteni akiwagawia wakulima wa Makete mbegu bora kwa ajili ya kilimo mara baada ya kuwapa elimu ya namna ya kutumia mbegu hiyo ili wapate mavuno bora.
 
Mbegu bora na ya kisasa ya mahindi inayohimili hali ya hewa ya mikoa yote ya nyanda za juu kusini inayozalishwa na kampuni ya highland seed growers ya jijini Mbeya ambapo wakulima wa makete wamepewa bure kwa ajili ya majaribio.
 Mtangazaji wa Kitulo FM iliyopo Makete Conradi Mpila akipokea mbegu
Bwana shamba Iddi Kapteni akitoa maelekezo kwa wakulima wa Makete namna ya kutumia mbegu hiyo ili iwapatie mazao mazuri
 Iddi Kapteni akionesha vipimo katika shamba darasa lililoandaliwa kwa ajili ya kuwafundisha wakulima wa Makete
 Msambazaji wa mbegu hizo Bw. Award Mpandila akitoa nasaha zake kwa wakulima wa Makete waliohudhuria shamba darasa
 Msambazaji wa mbegu Tito Tweve ambaye ni wakala aliyeidhinishwa na kampuni ya Highland na halmashauri ya wilaya ya Makete akionesha viashiria vya kutambua mbegu halisi na feki
 Mkulima Jeita Mahenge kutoka kijiji cha Isapulano Makete akifurahia baada ya kupewa mbegu bure
 Kaimu afisa kilimo mifugo na ushirika wilaya ya Makete Beda Kusenge akizungumza namna walivyojipanga kuzuia uingizaji wa mbegu feki za kilimo wilayani mwake
 Mwakilishi wa afisa pembejeo wilaya ya Makete Lazaro Moses akiwahakikishia wakulima hao kuwa pembejeo za kilimo kwa mwaka huu tayari zimefika Makete kwa wakati
Wakulima wakifurahia mbegu walizopewa bure


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo