HARUSI YA MSANII NATASHA YA KUKUMBUKWA

susan Lewisy
Natasha akiwa na Neeema msimamizi wa Harusi yake.

ILIKUWA ni siku ya kipekee katika historia ya tasnia ya filamu pale mwanadada na mdau mkubwa katika tasnia ya filamu Susan Lewisy ‘Natasha’ alipofunga pingu za maisha na Mr. Alex Humba katika kanisa la Mt. Joseph tarehe 27/7/ 2013 saa sita mchana tofauti na harusi nyingine ambazo zimezoeleka zinazofanyika kila uchwao.

susan lewisy
Natasha akiwa katika shera.
Monalisa akiwa na mdogo wake. 
Baada ya harusi hiyo ya kipekee kufungwa na kuhudhuriwa na waheshimiwa mbalimbali wakiwepo wasanii, maharusi walitoka na kuelekea Hotelini kwa ajili ya upigaji wa picha sambamba na kupumzika kabla ya kwenda ukumbini kwa ajili ya kusherekea ukumbi wa kisasa wa Magereza uliopo Ukonga.

Mr & Alex walipendeza kupita maelezo kwani kitu kilichowafanya wapendeze zaidi ilikuwa ni tabasamu lao sambamba na mavazi waliyovaa kwa siku hiyo maalumu kwao na kwa marafiki zao waliofika kwa kumsupport Natasha kama rafiki kipenzi wa jamii nzima ya tasnia ya filamu Swahiliwood, walipendeza sana na kuandika Hitoria ya maisha mapya.

Alex Humba, Susan Lewisy, S Mwakifwamba, Yvonne Cherryl
Maharusi wakiwa katika nyuso za furaha na Rais wa TAFF Mwakifwamba.
Yvonne Cherryl, Jamila, jalila, Sonia
Monalisa akiwa na wapambe wajukuu.
Susan Lewisy Neema
Natasha akiwa na Neema msimamizi wake.

Sherehe hizo zilipambwa na msafara wa mastaa wanaokuja kwa kasi katika tasnia ya filamu Bongo Jalila na Jamira wakiwa na Sonia binti Tyson wakiongozwa na mwigizaji nyota na maarufu asiyechuja Afrika Yvonne Cherryl aka Monalisa ambaye pamoja na umakini alipendeza kweli kweli na kuwa ni pambo la Harusi ya Natasha na kuwaziba midomo wale wote waliokuwa wakikejeli ndoa hiyo.

Uongozi wa FC unatoa pongezi kwa maharusi wetu Mr & Mrs Alex kwa kuungana na kuwa mwili mmoja na si wawili tena, Mungu abariki maisha yao ya ndoa Takatifu iliyofungwa na Mungu. Ameni. 

Natasha ni kiungo muhimu sana katika tasnia ya filamu Swahiliwood kwa mawasiliano na mwongozo pia kwa wasanii wote.

Ceo FC Myovela M.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo