DAR ES SALAAM YAONGOZA ZOEZI LA KUTEKETEZA KUNGURU WEUSI




Na Juma Mtanda, Morogoro.
JUMLA ya kunguru weusi 482,183 wameuawa katika kipindi cha miaka mitatu katika mikoa minee tangu kuanza kwa mpango wa kudhibiti kunguru weusi na panya Tanzania ulioanza mwaka julai 2010 hadi januari 2012.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Morogoro Mtaalam wa kudhibiti kunguru weusi na panya Tanzania, Adili Ngujiy alisema kuwa jumla ya kunguru weusi 482,183 tangu kuanza kwa mpango wa kuwadhibiti.
Ngujiy alisema kuwa kunguru hao wameuawa katika vipindi tofauti kati ya julai mwaka 2010 na januari 2012 kwa njia mbili tofauti za kuwekewa sumu na mitengo ambapo kat
ika jiji la Dar es Salaam limefanikiwa kuuawa kunguru 22,894 huku jiji la Tanga likiua kunguru 3216 wakati Kibaha likiwaua 1268.
“Tangu kuanza kwa mradi wa kuua kunguru Tanzania ulianza mwaka 1996 kuwatega kwa mitego pekee kwa jiji la Dar es Salaam na mwaka 2006 iliongezwa mbinu ya kuwaua kwa kutumia sumu katika programu iliyokuwa ikiendeshwa na wizara ya maliasi na utalii pekee” alisema Ngujiy.
Aliongeza Ngujiy kwa kusema kuwa baada ya kupata mafanikio programu ya kuua kunguru hao iliongezwa mikoa mingine mingine mitatu ikiwemo Morogoro, Pwani na Tanga baada ya kupata ufadhili wa mashirika ya Danida, Finida na USA chini ya wizara ya maliasili na utali.
Alitaja idadi ya mitego ya kuua kunguru hao katika mikoa hiyo kuwa Dar es Salaam pekee ina mitego 450, Tanga 20 na Kibaha 12 ambapo jumla ya kunguru imeua 27,378.
Kunguru waliouawa kwa njia ya kuwekewa sumu ni 464,181 ambapo Dar es Salaam imeua kunguru 306,772, Tanga 54,668, Pwani 15,078 na Morogoro 87,663 katika kipindi cha kuanzia julai 2010 mpaka februari 2012.
Ngujiy alisema kunguru 22,894 wenyewe waliuawa kutumia mitego 482 iliyotegwa katika miji ya Kihaba, Tanga huku Dar es Saalaam ikiwakilishwa na Temeke, Kinondoni na Ilala.
Kunguru hao wanadaiwa kuletwa na serikali ya uingireza kwa ajili ya kusafisha mji Mkongwe mwaka 1890 ambao kazi kubwa ni kula uchafu na kuingia Tanganyika wakati huo kuingia mwaka 1850 wakining’inia kwenye meli na maboti.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo