Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akiwasili Kigogo Mburahati, jijini Dar es Salaam, leo Julai 30, 2013
nyumbani kwa aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Juma
Haji Mkima, kwa ajili ya kutoa mkono wa pole kwa famili ya mhasibu huyo
aliyefariki dunia jana katika Hospitali ya Aga Khan. Marehemu Juma, anatarajia kuzikwa leo kijijini kwao, Rufiji.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akimfariji mke wa marehemu Juma Haji Mkina, Kibibi Juma Mkina,
aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, aliyefariki dunia
jana katika Hospitali ya Aga Khan, jijini Dar es Salaam. Makamu wa Rais
alifika nyumbani kwa marehemu Kigogo Mburahani leo Julai 30, 2013
kwa ajili ua kutoka mkono wa pole, kabla ya marehemu kusafirishwa kwenda
kuzikwa kijijini kwao Rufiji.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akijumuika pamoja na waombolezaji nyumbani aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa
Ofisi ya Makamu wa Rais, Juma Haji Mkina, aliyefariki dunia jana katika
Hospitali ya Aga Khan, jijini Dar es Salaam. Makamu alifika nyumbani kwa
marehemu Kigogo Mburahati, leo Julai 30 kwa ajili ya kutoa mkono wa
pole na kuwafariji wafiwa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiondoka Kigogo
Mburahati, jijini Dar es Salaam, leo Julai 30, 2013 nyumbani kwa aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Juma Haji Mkima, baada ya kufika kutoka mkono wa pole na kuwafariji wafiwa kutokana na msiba huo. Marehemu Juma, anatarajia kuzikwa leo kijijini kwao, Rufiji. Picha na OMR