Wananchi wa kata ya Iwawa wilayani Makete mkoani Njombe, wametakiwa kushiriki kikamilifu katika mchakato wa mapendekezo ya kugawa vijiji, na tarafa wilayani hapo, kabla ya julai 20 mwaka huu, ikiwa ni njia mojawapo ya kurahisisha maendeleo ya wananchi
Kauli hiyo imetolewa na diwani wa kata ya Iwawa Benjamin Mahenge wakati akizungumza na mtandao huu kuhusiana na suala hilo
Diwani Mahenge amesema hivi sana serikali imeona adha wanayoipata wananchi, huku akitolea mfano wa kata yake kuwa na kijiji cha Ndulamo ambacho ni kikubwa hivyo wananchi wake wanatakiwa kutoa mapendekezo hayo haraka
"Kijiji cha Ndulamo ni kikubwa sana, hakuna haja ya wananchi wake kuogopa kutoa mapendekezo, tayari nimeshawaambia kuhusu hilo na naimani watalifanyia kazi mara moja ili mapendekezo hayo yafike kunakohusika" alisema Mahenge
Hivi sasa wilaya ya Makete kwa ujumla ipo kwenye mapendekezo ya kugawa vijiji na tarafa kubwa kwa lengo la kurahisisha huduma za wananchi