Katibu tawala wilaya ya Makete Joseph Chota akisoma hotuba ya siku ya mazingira kwa mwaka huu katika kwa niaba ya mkuu wa wilaya Josephine Matiro, katika kata ya Isapulano wilayani Hapa
-----------
Wananchi wilayani Makete
wametakiwa kuhakikisha kuwa wanahifadhi mazingira kwa kuwa ni jambo muhimu
ambali litasaidia kuona raha ya kuishi kutokana na mazingira hayo kuzidi kuwa
mazuri
Rai hiyo imetolewa na mkuu wa
wilaya ya Makete mh Josephine Matiro katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba
yake na katibu tawala wilaya hiyo Bw. Joseph Chota katika maadhimisho ya siku
ya mazingira duniani yaliyoadhimishwa kiwilaya katika kata ya Isapulano
Amesema utunzaji wa mazingira ni
jambo zuri na la umuhimu hivyo kuwataka wananchi kutambua umuhimu huo wa
kuhifadhi mazingira, ikiwa ni pamoja na kutokata miti ovyo, kutupa taka ovyo
pamoja na shughuli zote ambazo zinaharibu mazingira
Matiro amesema ujumbe wa mwaka
huu unasisitiza kupunguza matumizi ya rasilimali zisizo rafiki na mazingira
pamoja na kupunguza au kuepuka uchafuzi wa mazingira, huku akisistiza kuwa
wananchi wakikubali kubadilika mazingira ya makete yatazidi kuwa mazuri siku
hadi siku
Kwa upande wao idara ya maliasili
wilaya ya Makete imesema jutihada zinaendelea kufanywa na idara hiyo kuhusu
utunzaji wa mazingira ambapo wanaendelea kutoa elimu kuhusu kulinda na
kuhifadhi vyanzo vya maji pamoja na kupanda miti ambayo ni rafiki na mazingira
ikiwemo Mivengi na Mitulunga
Wamesema kwa msimu wa mwaka
2012/2013 zaidi ya miti laki 8 imepandwa wilayani Makete huku lengo la wilaya
lilikuwa ni kupanda miti milioni 9 na wameshindwa kupata uhakika kama lengo
hilo limefikiwa kutokana na baadhi ya kata 6 ikiwemo Isapulano ambayo
maadhimisho hayo yamefanyika, kushindwa kufikisha taarifa za upandaji miti
kwenye ofisi ya maliasili na mazingira kwa wakati, ila wanaamini lengo hilo
limefikiwa
Maadhimisho ya siku ya mazingira
duniani huadhimishwa kila tarehe 5, Juni ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni
fikiri kabla ya kula, hifadhi mazingira