WANACHAMA WA CCM WAFANYA HARAMBEE YA KUKOMBOA KIWANJA CHAO

Wanachama wa chama cha mapinduzi tawi la Ikonongo kata ya mkwawa manispaa ya Iringa  wamefanya harambee kwa ajili  ya kukomboa kiwanja ambacho walitakiwa kujenga ofisi ya chama chao.
  
Akizungumza katika harambee hiyo  Mwenyekiti wa tawi AMRI KALINGA amesema kuwa ujenzi huo umeshindwa kufanyika mapema kutokana na kiwanja hicho kuwa na mgogoro ila kwa sasa wameshafikia muafaka na tayari wamelipa fidia ya shilingi laki tano na nusu.
  
Naibu meya wa manispaa GERVAS NDAKI ambaye alikuwa mgeni rasmi katika harambee hiyo amewataka wananchi hao kuwa wabunifu kwa vitu ambavyo vitawasaidia kuwainua kiuchumi katika kijiji chao na sio kuishia kujenga ofisi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo