NYALANDU: TEMBO 10,000 HUUAWA KILA MWAKA HAPA NCHINI

Naibu wa Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu imesema serikali inaanda oparesheni maalumu ya kupambana na watu wanaojihusisha na vitendo vya ujangili katika hifadhi za taifa kwa kuwa vinatishia hali ya usalama wa nchi.
 
Akizungumza wakati wa  uzinduzi wa mkutano wa wadau wa Ulinzi  wa Maliasili katika hifadhi za taifa zilizopo mikoa ya nyanda za juu kusini Nyalandu alisema vitendo vya ujangili hususani vinavyohusisha  na uwindaji haramu na uuaji wa Tembo vinatisha kutokweka kwa wanyama hao nchini.
 
Alisema tafiti zilizopo zinaonesha kuwa kwa sasa Tembo 10,000 wanauawa katika kila mwaka hapa nchini  na kuongeza kuwa idadi hiyo ni kubwa na kama itachwa iendelee Tembo waliopo nchini ambao wanafikia 140,000 watatoweka.
 
“Serikali imeweka mkakati malaumu wa kupambana na vitendo hivyo,kwanza tunafanya mabadiliko makubwa  katikasheria zetu suala zima la utoaji adhabu kwa watu watakaobainika kujihisha na vitendo hivyo…wito wangu kwa wanachi  wanajihusisha na kazi hiyo kuacha mara moja na watu wote kushiriki katika shughuli za  ulinzi wa Maliasili za Taifa”alisema Nyalandu.
 
Nyalandu alifafanua kuwa vitendo vya ujangili katika maeneo ya hifadhi kwakiwango kikubwa vinatekelezwa na watu  ambao hushirikiana na watumishi katika idara mbalimbali za serikali na mamlaka zinazofanya kazi katika hifadhi hizo na kuongeza kuwa katika mkakati ulipo kila atakayebainika kuanzi sasa atatangazwa hadharani na kuchukuliwahatua kali bila kujali wadhifa wake.
 
Alitaja makundi ya watu wanaofanya kazi katika maeneo ya hifadhi za Taifa,Viwanja vya Ndege,Bandarini na idara za uhamiaji walioko katika maeneo ya mipakani kuwa  baadhi yao  wanaoshiriki katika vitendo hivyo vya ndiyo sababu pembe za ndovu kutoka hapa nchini husafirishwa hadi nje ya nchi bila ya kukamatwa .
 
“Isingewezekana mtu aingie kwenye hifadhina kuoa Tembo hadi anafiisha idadi ya meno yanye kujaza loli kisha afukie chini na kutafuta gari la kubeba Meno hayo bila ya kujulikana,mtu huyo ni lazima ashirikiane na baadhi ya watu katika makundi haya, …,natoa wito kwa wafanyakazi katika hifadhi za Taifa,viwanjwa vya Ndege,Bandarini na wale walioko mipakani kuacha kushirikiana na majangili kwani watakaobainika serikali hawaitawahurumia”alisema Nyalandu.
 
Alitaka watu wote wanaomiliki silaha kinyume na sheria za nchi kuzisalimisha kabla ya mchakato na hatua kali za kisheria hazichukuliwa dhidi yao kwa kuwa silaha hizo haramu zimekuwa zikitumika katika kutekeleza vitendo vya uharifu katika hifadhi za Taifa.
 
Kuhusu majangili kutumia silaha kali alisema serikali inafanya majadiliano na nchi mbalimbali kuona njia sahihi za kupambana na majangili hao kwa lengo la kunusuru wanyama hao hususani Tembo ambao kwa sasa idadi yao imepungua sana.
 
Nyarandu alitajasababu za kukithiri kwa vitendo vya uhalifu huo kuwa zinatokana na ongezeko la matumizi ya pembe za Ndovu na soko kubwa lililopo katika baadhi ya nchi hususani za bara la Asia.
 
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Tanapa Taifa Alan Kijazi alisema mkutano huo ulioandaliwa na Mradi wa kuboresha Mtandao wa Ulinzi wa Hifadhi za malisili  katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini umelenga kukusanya maoni ya namna ya kupambana na ujangili kufutia oongezeko la ujangili katyika hifadhi za Taifa.
 
Alisema mkutano huo wa siku mbili utajadili hatua za kuchukua katika kupambana na vitendo hivyo na kisha kuunda kikundi kazi kwa ajili ya kukabiliana na vitendo vya ujangili katika hiafadhi zilizpo katika miko ya nyanda za juu kusini.
 
Mkutano huo ulihudhuriwa na wakuu wa mikoa kutoka mikoa ya Nyanda za juu kusini na pia na wakuu wa wilaya zote toka katika maeneo hayo.
Na Berdina Majinge, Iringa


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo