MOTO WAZUKA NA KUTEKETEZA CHUMBA IRINGA

Moto mkubwa umezuka jana na kuunguza chumba kimoja katika maeneo ya kibwabwa Ipogolo kata ya Ruaha manispaa ya Iringa.
 
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo  kamanda wa polisi mkoa wa iringa RAMADHANI  MUNGI amesema moto huo umezuka katika nyumba ya HIRALI  RAMADHAN ambayo ilikuwa na wapangaji.
 
Amesema chumba hicho kilikuwa kinakaliwa na CHRISTINA MFUGA na moto huo haukuwa na madhara yoyote kwa binadamu kwani kikosi cha zima moto kiliwahi kufika katika eneo la tukio.
 
Aidha amesema kuwa jeshi la polisi bado linaendelea kufanya uchunguzi ili kubaini chanzo cha moto huo pamoja na gharama za vitu ambavyo vimeteketea.
 
WAKATI HUO HUO.

Mtu mmoja aliyefahamika  kwa jina la JOJINA  KABOGO(29) anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani  Iringa kwa uchunguzi zaidi kufuatia tukio la kuokotwa kwa mtoto mchanga mkoani hapa.
 
Tukio hilo limetokea  katika maeneo ya mlandege manispaa ya iringa ambapo  afisa mtendaji wa mtaa huo FADHILI OSKA amemuokota mtoto huyo anayekadiriwa kuwa na umri wa miezi 6 jinsi ya kiume akiwa ametupwa jalalani.
 
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa iringa RAMADHANI MUNGI amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa uchunguzi bado unaendelea na kosa hilo ni la jinai, na ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa iringa kuacha tabia hiyo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo