Mbunge wa Mtwara Mjini, Hasnein
Murji (pichani) ametiwa mbaroni na Jeshi La Polisi kwa tuhuma za uchochezi na
kuhusika katika vurugu zilizotokea hivi karibuni katika viunga vya mji
wa Mtwara.
Habari zilizoifikia blog hii usiku huu zimeeleza kwamba mbunge huyo amekamatwa saa 2:30 usiku huu na anashikiliwa katika kituo Kikuu cha Polisi Mjini Mtwara.
Katibu wa Mbunge huyo Meckland Millanzi amethibitisha kukamatwa kwa Murji na kwamba anahusishwa na mvurugu hizo.
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Advera Senso amesema kwamba Murji amekamatwa usiku huu nyumbani kwake katika eneo la Shangani.
Taarifa zimebainisha kwamba Murji amekamatwa na kwamba hati ya kumkamata imeeleza anatuhumiwa kuchochea vurugu za kupinga gesi ya Mtwara kwenda jijini Dar es Salaam.
Mpaka sasa watu zaidi ya 80 wamekamatwa na jeshi la polisi na kushtakiwa mahakamani.
Habari zilizoifikia blog hii usiku huu zimeeleza kwamba mbunge huyo amekamatwa saa 2:30 usiku huu na anashikiliwa katika kituo Kikuu cha Polisi Mjini Mtwara.
Katibu wa Mbunge huyo Meckland Millanzi amethibitisha kukamatwa kwa Murji na kwamba anahusishwa na mvurugu hizo.
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Advera Senso amesema kwamba Murji amekamatwa usiku huu nyumbani kwake katika eneo la Shangani.
Taarifa zimebainisha kwamba Murji amekamatwa na kwamba hati ya kumkamata imeeleza anatuhumiwa kuchochea vurugu za kupinga gesi ya Mtwara kwenda jijini Dar es Salaam.
Mpaka sasa watu zaidi ya 80 wamekamatwa na jeshi la polisi na kushtakiwa mahakamani.