SONY DSC
WADAU TUNAOMBA RADHI KWA PICHA HII KAMA ITAKUKWAZA LAKINI NDIO UNYAMA WA BINADAMU WA SASA….KUNA WANAOKESHA USIKU KUCHA WAKIMLILIA MUNGU AWAJALIE KUZAA LAKINI WENGINE WANATUPA WATOTO WASIOKUWA NA HATIA…Pichani ni Maiti ya kitoto kichanga ikiwa kwenye mfuko wa rambo.
SONY DSC
Wakazi wa eneo la Magomeni zilipovunjwa nyumba za KOTA jijini Dar es salaam leo wakishuhudia mtoto mchanga anayekadiriwa kuwa umri wa siku moja akiwa ametupwa huku akiwa amekufa katika eneo hilo na mtu asiyefaamika. (Picha na Philemon Solomon wa Fullshangwe).
SONY DSC
Gari la askari polisi wa kituo cha Magomeni usalama wakiwa  katika eneo ambalo ametupwa mtoto mchanga akiwa amekufa kwa ajili ya kuchukua mwili wake na kumpeleka sehemu husika.
SONY DSC
Maiti ya Kitoto kichanga kinachokadiriwa kuwa na umri wa siku moja ikiwa imepakiwa kwenye gari la polisi.
SONY DSC
Wakazi wa jirani na eneo hilo wakiwa wamekusanyika eneo la tukio. (Picha na Mo Blog)