KIONGOZI WA CUF ATIWA MBARONI KWA TUHUMA ZA VURUGU MTWARA

2
Habari kutoka ndani ya Jeshi la Polisi nchini zinasema kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana wa Chama cha CUF, Katani Ahmed Katani, ametiwa nguvuni jijini Dar es Salaam akituhumiwa kuhusika na uchochezi wa vurugu ambazo zimekuwa zikitokea mkoani Mtwara. 

Katika kutafuta ukweli wa habari hii Mwandishi wetu aliwasiliana na viongozi kadhaa wa CUF, akiwemo Julius Mtatiro ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa CUF, ambao walithibitisha kukakamatwa kwa Bwana Katani na kuwa tayari amekwishasafirishwa kwendaMtwara.
 
Taarifa kutooka ndani ya chama cha CUF zimethibitisha zaidi kuwa Katani alipigiwa simu na maofisa wa polisi wa Kituo Kikuu na kuelezwa kuwa anatakiwa afike kituoni hapo kwa mahojiano ambapo mara baada ya kufika alitiwa nguvuni na kuanza kuhojiwa.

Itakumbukwa kwamba ni muda mrefu sasa kumekuwa kunatokea vurugu Mtwara zinazohusiana na wananchi kupiga mradi wa bomba la gesi kutoka mkoani humo kwenda Dar es Salaam. Hadi sasa vurugu hizo zimesababisha vifo vya watu na uharibifu wa mali za serikali, viongozi na raia.

Kufuatia matukio hayo serikali ilitangaza kuwasaka watu wote watakaothibika kuhusika na vurugu hizi ambazo kwa ujumla zinaitia doa nchi yetu.

credits dar24


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo