Katikati ni Diwani wa Kata ya Lupembe Bi.Twilumba Wapalila[Picha wakati wa Baraza la Madiwani toka Maktaba yangu.]
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa
Wilaya ya Njombe Bwana Lupyana Fute[Jacky's]Aliyevalia Shati la CCM
Ambaye Pia ni Diwani wa Kata ya Njombe Mjini awali aliuagiza uongozi wa
Kijiji kuwasomea Wananchi Taarifa ya Mapato na Matumizi Kila baada ya
Miezi Mitatu Jambo ambalo halitekelezeki.
Na Michael Ngilangwa.
Wananchi wa Kijiji Cha Lupembe Barazani
Wilayani Njombe Wameikataa Taarifa ya Mapato na Matumizi Iliosomwa na
Uongozi wa Kijiji Hicho Wakati wa Mkutano Uliofanyika Kijijini Humo,Kwa
Madai ya Taarifa Hiyo Kuwa na Mapungufu Mengi.
Miongoni Mwa Mapungufu Hayo ni Pamoja na Taarifa Hiyo Kutoaninisha Kikamilifu Kuhusu Matumizi ya Fedha Za Kijiji Pamoja na Wananchi Kutokubaliana na Mchanganuo wa Fedha Hizo Kama Ulivyoaninishwa na Viongozi Wakati wa Mkutano Huo.
Miongoni Mwa Mapungufu Hayo ni Pamoja na Taarifa Hiyo Kutoaninisha Kikamilifu Kuhusu Matumizi ya Fedha Za Kijiji Pamoja na Wananchi Kutokubaliana na Mchanganuo wa Fedha Hizo Kama Ulivyoaninishwa na Viongozi Wakati wa Mkutano Huo.
Aidha Kutokana na Hali Hiyo,Uongozi wa Kijiji Ulilazimika Kurudisha Kiasi Cha Shilingi Millioni Mbili Ambazo Hazikuweza Kupatiwa Majibu ya Kina Licha ya Wananchi Kuhoji Mara Kadhaa Kuhusu Fedha Hizo Ambazo Zilitengwa Kwaajili ya Kuboresha Miundombinu ya Maji.
Akizungumza na blog hii ,Diwani wa Kata ya Lupembe Bi Twilumba Wapalila Amesema Baada ya Kuahirishwa Kwa Mkutano Huo Sasa Mkutano Mwingine Utafanyika Jumamosi Wiki Ijayo na Kuongeza Kuwa Wanatarajia Kuzisoma Taarifa Zote Kama Ilivyoelekezwa na Wananchi na Viongozi Mbalimbali wa Chama na Serikali.
Akiwa Kwenye MKutano wa Hadhara Wakati wa Ziara ya Kutembelea Vijiji Vya Tarafa ya Lupembe,Mjumbe wa NEC Taifa Wiilayani Njombe Bw Lupyana Fute Aliuagiuza Uongozi wa Kijiji Hicho Kuhakikisha Unawasomea Wananchi Taarifa za Mapato na Mtaumizi Hadi Kufikia May 18 Mwaka Huu na Kusema Kinyume na Hapo Hatua za Kisheria Zingeweza Kuchukuliwa Kwa Viongozi Hao
Kumekuwa na Hali ya Viongozi wsa Vijiji Mkoani Njombe Kukiuka Sheria za Serikali za Mitaa Zinazowataka Kuwasomea Wananchi Taarifa za Mapato na Matumizi Kila Baada ya Miezi Mitatu Jambo Ambalo Limekuwa Likisababisha Migogoro ya Mara Kwa Mara Baina ya Wananchi na Viongozi Wao.