DC MAKETE: WAZAZI WA WATOTO WALIOSHINDWA KURIPOTI KIDATO CHA KWANZA 2013 KUKIONA


Makete

Wilaya ya Makete mkoani Njombe imejipanga kuhakikisha inawachukulia hatua za kisheria wazazi wa wanafunzi ambao hawajaripoti shuleni hasa wa kidato cha kwanza, kutokana na wazazi wengi kuwa ndiyo sababu inayopelekea wanafunzi hao kutofika shuleni

Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Makete mh Josephine Matiro wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za serikali kwa kipindi cha Januari-Aprili 2013 katika wilaya yake

Matiro amesema amegundua wapo baadhi ya wazazi wa Makete ambao huwatorosha watoto wao na kwenda kuwapeleka kufanya kazi hasa za ndani nje ya wilaya yake ilihali watoto hao walifaulu kwenda kidato cha kwanza

“Wazazi mnatakiwa kufahamu urithi wa mtoto ni elimu na inasikitisha sana kama humpeleki mtoto wako shule ili akawe housegirl au houseboy mijini, naimani watoto hao lazima waje kuwalaumu nyie wazazi kwa kutompa elimu” alisema Matiro

Amesema kwa hivi sasa tayari wameanza kuushirikisha uongozi wa kata na vijiji kuwasaka wazazi na walezi wa watoto ambao hawajaripoti shuleni ili kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria

Jumla ya wanafunzi 2,173 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wilaya ya Makete mwaka huu 532 hawajajiunga na masomo hayo hadi sasa

Taarifa hiyo ya mkuu wa wilaya iligusa Nyanja mbalimbali ikiwemo, Elimu, afya, maji, kilimo, barabara, maliasili na utalii
Na Edwin Moshi, Makete


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo