Wilaya ya Ludewa
Na Nickson Mahundi
Mtoto wa
jinsi ya kiume amenusurika kifo wilayani Ludewa katika mkoa wa Njombe baada ya
kuzaliwa na kutupwa porini na mama yake jirani na makazi ya watu na kuokotwa na
raia wema ambapo walimuwahisha hospitali ili kuokoa maisha yake.
Akiongea na
waandishi wa habari Muuguzi wa zamu katika hospitali ya wilaya ya Ludewa Bi.Eda
Muhema alisema alimpokea mtoto huyo kutoka kwa wasamaria wema waliotokea Ludewa
Kijijini mtaa wa songambele majira ya jioni Februari 28 mwaka huu akiwa katika
hali nzuri kutokana na wasamaria hao kumsitiri kwa nguo nzito.
Bi.Muhema
alisema mtoto huyo aliletwa akiwa na uzito wa kilo tatu na akiwa ameshakatwa
kitovu kwa kutumia panga hivyo alichokifanya yeye ni kukipunguza kitovu hicho
na kumtengeneza kitaalamu zaidi.
“tumempokea
akiwa salama kama mnavyomuona lakini inaonekana amezaliwa usiku na kapigwa na
baridi lakini kutokana na umahiri wa akinamama waliomuokota waliweza kumpa
huduma ya kwanza na kufunika nguo nzito ili kumsaidia kurudisha joto lake la
mwili,”alisema Bi.Muhema.
Kwa mujibu
wa shuhuda mmoja wa tukio hilo aliyejitambulisha kwa jina moja la Mrs.Kidulile
ambaye ni muuguzi mstaafu alisema ilikuwa ni majira ya jioni februari 28 mwaka
huu aliona wanafunzi wakishangaa kitu katika shamba la mahindi.
Ndipo
alipowauliza kunani hapo nao wakamjibu kuwa kuna kitoto kichanga kimetupwa hapa
alisema kutokana na taaluma yake alifika eneo la tukio na kubaini kuwa mtoto
huyo alikuwa bado yuko hai,akawaita wanawake wenzie na kuchukua nguo ili
kumfunika.
Mrs.Kidulile
alisema mtoto huyo alitupwa jirani na makazi ya watu ambapo palikuwa na maji
yakitiririka kutoka katika bomba lililo pasuka lakini maji hayo hayakuweza
kumfikia alipolazwa.
Alisema
walimkuta mtoto huyo akiwa hajakatwa kitovu na akiwa kaviringishwa katika gunia
hivyo walilazimika kumkata kitovu kwa kutumia panga alilobeba mama mmoja
aliyekuwa akienda shambani na kumuwahisha hospitali ili ahifadhiwe vizuri.
Katika kuulizia kwa wajirani ndipo walipompata
mwanamke aliyemtupa huyo mtoto wakamchukua na kumfikisha katika kituo hicho cha
polisi cha Ludewa mjini ambako mwnamke huyo anaendelea kushikiliwa na jeshi la
Polisi.
Aidha mama
huyo Bi.Magdarena Lugongo anayetuhumiwa kwa kosa la kumzaa mtoto na kumtupa
akihojiwa na waandishi wa habari alikiri kutenda kosa hilo na kueleza sababu
kubwa ni ugomvi ndani ya ndoa.
Bi.Magdalena
alisema alifanya uamuzi huo kutokana na hasira kwani mume wake aliye mtaja kwa
jina la Andrea Kayombo aliukataa ujauzito huo kuwa sio wake na kumpa manyanyaso
makubwa pindi ana ujauzito.
