WANAFUNZI WAMALIZA MGOGORO WA GEREJI BUBU


images 
WANAFUNZI wa Shule ya Msingi ya Dk. Omari Juma, wamemtaka Mwanasheria wa Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam kumaliza mgogoro wa gereji bubu zinazozunguka shule hiyo.
 
Wakizungumza na waandishi wa habari katika eneo la shule hiyo, wanafunzi hao walisema kama kero yao haitasikilizwa haraka, kinyume chake wataandamana hadi kwa mkurugenzi wa manispaa hiyo.
 
Walisema uwepo wa gereji hizo ukichanganyika na uvunjifu wa maadili kwa kuwasumbua watoto wa kike, kumekuwa kukishusha taaluma ya wanafunzi wa shule hiyo.
 
Mmoja wa wanafunzi hao, Ever Joseph, alisema wamekuwa wakishindwa kuzingatia masomo kutokana na makelele ya vyuma wakati wa matengenezo ya magari.
 
Naye Yusufu Saidi, alisema wanasikitishwa na mafundi hao kutumia lugha za matusi wakati wanaporuka ukuta kwa ajili ya kwenda kujisaidia katika choo cha shule hiyo.
 
Alisema wakati mwingine inatokea magari yanasababisha ajali kwa kugonga ukuta wa shule hiyo, kitendo kinachotishia maisha ya wanafunzi hao.
 
“Mazingira haya yanachafuliwa hovyo, kama mnavyoona shule yetu yote imezunguukwa na gereji, mafundi seremala na mafundi nguo ambao wote hao wamekuwa wakijiingiza katika vitendo vya udanganyifu wa kimapenzi kwa dada zetu na kuwapotosha kielimu,” alisikitika Saidi.
 
Naye Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Triphonia Kahwili, aliomba serikali kuingilia kati mgogoro huo ili kila mmoja kati ya shule hiyo na wamiliki wa gereji kufanya kazi zao kwa kufuata sheria


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo