Chama cha mapinduzi(CCM) wilayani Makete kimedhamiria
kuendelea kuibana serikali wilayani humo kuhakikisha inatoa huduma bora kwa
wananchi wake kama ilivyo adhma ya serikali ya
kutoa huduma bora kwa wananchi wake
Akizungumza na mtandao huu ofisini kwake katibu wa CCM
wilaya ya Makete Miraji Mtaturu amesema kwamba kwa mujibu wa taarifa ya
utekelezaji wa ilani ya chama chake kwa kipindi cha mwaka mmoja 2011/2012
iliyosomwa na serikali katika kikao cha halmashauri kuu ya CCM wilaya ya
Makete, wao kama chama wamegundua kuwa bado kuna kusuasua katika utekelezaji wa
miradi ya kilimo, afya, miundombinu na utawala bora
Amesema ingawa kuna uhaba wa wagani kazi katika sekta ya
kilimo lakini hao waliopo baadhi yao
hawatendi kazi zao ipasavyo hali ambayo inapelekea usumbufu kwa wananchi
hususan wakati wa kupatiwa pembejeo za kilimo
“Kwa mfano pale kwenye kata ya Isapulano tumeelezwa wakala
ameleta mbolea muda mrefu lakini bado hajaisambaza kwa wananchi, sisi tumeagiza
kupitia kikao kile kuwa halmashauri kupitia idara ya kilimo ilifuatilie hilo mapema kabla msimu
haujapita, na pia afisa kilimo wa kata hiyo anaonesha uzembe mahali Fulani”
alisema Mtaturu
Kata hiyo ambayo pia inachangamoto ya barabara kutopitika
Mtaturu amesema kikao hicho kimemuagiza mkurugenzi mtendaji wa wilaya ya
Makete, kuhakikisha barabara hiyo inapitika na kuwatolea adha wananchi ambao
huitumia kusafiri kwenda mkoani Mbeya
“mkurugenzi alitueleza kuwa fedha ya matengenezo ya barabara
hiyo ipo na mkandarasi ameshapatikana lakini kinachosubiriwa ni msimu wa mvua
upite ndipo matengenezo yafanyike lakini sisi kama chama tumemtaka mkurugenzi
na mhandisi wa ujenzi wilaya kufanya maarifa na matengenezo madogomadogo ya
mashimo hayo ili barabara hiyo ipitike wakati huu wa masika ili iwasaidie
wananchi” alisema
Kuhusu suala la afya kikao hicho kimeiagiza serikali
kuhakikisha inaendelea kutoa elimu ya watu kujiunga na mfuko wa afya ya jamii
(CHF) ambapo bado kuna maeneo mengine wananchi wamekuwa wagumu kuchangia kumbe
hali hiyo inasababishwa na wao kutokuwa na uelewa wa kutosha kuhusu elimu hiyo
Mtaturu amesema pia suala la matibabu bure kwa wazee nalo
litiliwe mkazo kwani kumezkuwa na malalamiko kutoka kwa wazee wengi kuwa bado
wanatozwa fedha pindi wanapokwenda kupatiwa matibabu ilihali wana miaka 60 na
kuendelea
