BARABARA YA OLD BAGAMOYO SASA KUITWA MWAI KIBAKI

Barabara iliyokuwa ikijulikana kwa jina la Old Bagamoyo kuanzia leo itaanza kuitwa jina la 'Mwai Kibaki road' ikiwa ni heshima kwa aliyotunukiwa rais huyo wa Kenya kwa ziara yake ya siku mbili nchini hapa.

Mkuu mkoa wa Dar es salaam Meck Sadik amesema barabara hiyo yenye urefu wa Km 10.1 ni kuanzia kwenye mataa ya Morocco hadi mzunguko wa kuelekea Africa Mbezi beach mkabala na uwanja wa JWTZ.

Pia Rais Mwai Kibaki atatumia fursa hiyo kuwaaga na kuwashukuru watanzania kwa ushirikiano wao kipindi cha uongozi wake maana muhula wa uongozi wake unaelekea kikomo hapo baadaye mwaka huu.

SOURCE: issamichuzi.blogspot.com


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo