skip to main |
skip to sidebar
BARABARA YA OLD BAGAMOYO SASA KUITWA MWAI KIBAKI
Barabara
iliyokuwa ikijulikana kwa jina la Old Bagamoyo kuanzia leo itaanza
kuitwa jina la 'Mwai Kibaki road' ikiwa ni heshima kwa aliyotunukiwa
rais huyo wa Kenya kwa ziara yake ya siku mbili nchini hapa.
Mkuu mkoa wa Dar es salaam Meck Sadik amesema barabara hiyo yenye urefu
wa Km 10.1 ni kuanzia kwenye mataa ya Morocco hadi mzunguko wa kuelekea
Africa Mbezi beach mkabala na uwanja wa JWTZ.
Pia Rais Mwai Kibaki atatumia fursa hiyo kuwaaga na kuwashukuru
watanzania kwa ushirikiano wao kipindi cha uongozi wake maana muhula wa
uongozi wake unaelekea kikomo hapo baadaye mwaka huu.
SOURCE: issamichuzi.blogspot.com
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi