AISHA BUI ASUBIRIA OPARESHENI YA MATITI YAKE SAUZI!

Na Imelda Mtema
MSANII wa filamu ambaye amekuwa kimya kwa muda mrefu, Aisha Bui amesema kuwa kwa sasa anasubiria muda wa kufanyiwa upasuaji wa matiti yake kabla ya kurejea kwenye fani.
 
 
Aisha Bui.
Akizungumza hivi karibuni, Aisha alisema kuwa zoezi la upasuaji huo litafanyika  Machi mwaka huu huko Afrika Kusini lengo likiwa ni kutengeneza muonekano anaoutaka.

“Nimekuwa na muonekano nisioupenda, sipendi haya matiti makubwa ndiyo maana nimeamua kufanya upasuaji, nimeambiwa inawezekana na nitafanya hivyo mwezi wa tatu,” alisema Aisha na kuongeza:

“Najua wapo wanaojiuliza niko wapi, nimejichimbia huku Sauzi na nikirejea sanaa kama kawa.”
NA GPL


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo