
Waziri Mkuu
Mizengo Pinda akimweleza jambo Meneja wa Takwimu za Kilimo Bi. Joyce
Urassa alipotembelea Ofisi ya Taifa ya Takwimu jijini Dar es salaam.

Mkuu wa Kitengo cha Ramani Ofisi ya Taifa ya
Takwimu Vincent Mgaya (kushoto) akitoa ufafanuzi kwa Waziri Mkuu Mizengo
Pinda kuhusu matumizi ya ramani kupata Takwimu za Kilimo, Uchumi na
Utalii.

Meneja wa Idara ya Pato la
Taifa wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bw. Daniel Mwasula akitoa ufafanuzi
kwa Waziri mkuu Mizengo Pinda kuhusu Pato la Taifa na namna ofisi yao
inavyofanya kazi kukokotoa pato la taifa.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiwa katika Picha ya
Pamoja na viongozi na watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu mara baada
ya kukamilisha ziara yake. Picha zote na Aron Msigwa – MAELEZO.