MBUNGE WA KINONDONI AAHIDI KUISAIDIA FAMILIA YA SAJUKI


Kutokana na hali ya majonzi na masikitiko makubwa kwenye familia ya  marehemu Sajuki mbunge wa Kinondoni Iddi Azam ameahidi kuisaidia kwa hali na mali familia aliyoiacha marehemu Sajuki

Ahadi hizo alizisema juzi wakati alipofika nyumbani kwa marehemu kwa lengo la kutoa pole na salamu za rambirambi kwenye familia hiyo

Azam alisema kuwa anadeni kubwa kwenye familia hiyo pamoja na  mtoto aliyeachwa na marehemu, hivyo ni wajibu wake kumsaidia kadri ya uwezo wake

"Kila mtu anaiona hali ya Wastara sasa ilivyo basi sisi tulio baki tuwe kama Sajuki, kwani mapenzi walio kuwa nayo ni mfano wa kuigwa kwetu, hivyo nina jukumu la kuisaidia familia hii" alisema Azam

Aliongezea kuwa ni jukumu la kila mmoja wao kumuenzi marehemu Sajuki kwa vitendo Sajuki anazikwa leo katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo