MAMA AMUUA MWANAYE WA MIEZI 11

Kamanda wa Polisi kanda maalumu ya Tarime na Rorya Justus Kamugisha
JESHI la Polisi katika Kanda Maalumu ya Tarime na Rorya, linamshikilia Prisca Mwita mwenye umri wa miaka 22, mkazi wa Mtaa wa Nyamisangura, mjini Tarime, kwa tuhuma za kumuua mtoto wake mchanga na kumnyofoa baadhi ya viungo vyake.
 
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Tarime na Rorya, Justus Kamugisha, amesema kuwa, tukio hilo limetokea Januari 11, mwaka huu, majira ya saa 2:00 asubuhi nyumbani kwa mwanamke huyo.

Amesema kuwa, mwanamke huyo, anatuhumiwa kumuua mtoto wake, Happy Anthony, mwenye umri wa miezi 11, baada ya kumkata sikio la kushoto, kumnyoa nywele za upande wa kushoto, kumnyoa nyusi za jicho la kushoto na kumchuna ngozi ya kichwa sehemu ya kushoto.
 
Ameongeza kuwa, majirani wamegundua unyama huo na kutoa taarifa kwa viongozi wa eneo hilo, kitendo ambacho kimesaidia kutiwa mbaroni kwa mtuhumiwa.
 
Kufuatia tukio hilo, wananchi wa eneo hilo wamehusisha tukio hilo na imani za kishirikina, kwani ni la ajabu kwa mama mzazi kufanya unyama dhidi ya mtoto wake.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo