.
Na Francis Godwin
KATIBU wa chama cha
mapinduzi (CCM) wilaya ya Mufindi Jackob
Nkomola leo amefiishwa mahakamani akituhumiwa
kuua kwa maneno .
Akisoma shtaka hilo
linalomkabili katibu huyo mahakamani
hapo hakimu wa mahakama ya mwanzo Mafinga
wilayani Mufindi
Zakaria Mushi alisema
mtuhumiwa Jackob Nkomola anashtakiwa kwa kosa la kumtishia kumuua kwa maneno,
Alexandel Tweve kinyume na sheria
kifungu namba 89 kifungu kidogo “A”.
Aidha hakimu huyo alisema mshitakiwa alitenda kosa hilo, Octoba 3 mwaka 2012 katika eneo la Mkombwe, ambapo alimtishia mkazi huyo wa mji wa Mafinga wilaya ya Mufindi..
Mtuhumiwa alikana shtaka hilo na hakimu kutoa masharti ya dhamana ya ahadi ambayo inathamani ya shilingi 200,000 na adhaminiwe na mtu mmoja atakayetambulishwa kwa barua kutoka katika ofisi ya serikali ya kijiji au Kata masharti ambayo yalitimizwa na mshitakiwa na kesi hiyo itafikishwa tena mahakamani hapo Januari 30 mwaka huu.
Hakimu alimtaka mlalamikaji wa kesi hiyo kufika na mashahidi wake
aliowaorodhesha.
Aidha hakimu huyo alisema mshitakiwa alitenda kosa hilo, Octoba 3 mwaka 2012 katika eneo la Mkombwe, ambapo alimtishia mkazi huyo wa mji wa Mafinga wilaya ya Mufindi..
Mtuhumiwa alikana shtaka hilo na hakimu kutoa masharti ya dhamana ya ahadi ambayo inathamani ya shilingi 200,000 na adhaminiwe na mtu mmoja atakayetambulishwa kwa barua kutoka katika ofisi ya serikali ya kijiji au Kata masharti ambayo yalitimizwa na mshitakiwa na kesi hiyo itafikishwa tena mahakamani hapo Januari 30 mwaka huu.
Hakimu alimtaka mlalamikaji wa kesi hiyo kufika na mashahidi wake
aliowaorodhesha.
