Rais Jakaya Kikwete
NA FRANCIS GODWIN
WANANCHI
wa kata ya Ludende jimbo la Ludewa mkoani Njombe wadai toka nchi
ipate uhuru mwaka 1961 katika kata hiyo hawajapata kutembelewa na
Rais wala waziri japo wamekuwa wakibahatika kuona picha za Rais na
mawaziri kwenye magazeti pekee.
Wakizungumza
katika mkutano wa hadhara wa mbunge wa jimbo hilo la Ludewa Deo
Filikunjombe juzi wananchi hao walimwomba mbunge huyo kufikisha
ombi lao la kutembelewa na viongozi hao wa juu kwa Rais Jakaya
Kikwete ili ikiwezekana kabla ya kumaliza muda wake kuwatembelea
wananchi hao.
Fidelis Haule alisema kuwa yawezekana kata hiyo imeendelea kua
nyuma katika
maendeleo kutokana na viongozi wa ngazi ya juu serikali kuitenga
kata hiyo .
Alisema
kuwa kwenye kata hiyo ambayo wananchi wake wamekuwa wakilazimika
kutumia maji ya mto na madimbwi ya mvua kutokana na kutokuwa na
huduma ya maji safi na salama pia inakabiliwa na matatizo mbali
mbali likiwemo tatizo la daraja linalounganisha kijiji hicho na
vijiji vya jirani .
Haule
alisema kuwa viongozi wa Halmashauri ya wilaya hiyo ya Ludewa
wameendelea kuwa kikwazo kikubwa katika maendeleo ya kata hiyo na
wameendelea kukwama katika uzalishaji kutokana na utendaji mbovu wa
viongozi wao.
Kwani
alisema pamoja na
maeneo mengi ya wilaya hiyo wakulima wameanza kupalilia mahindi
yao ila katika kata hiyo baadhi ya wananchi bado hawajapanda mazao
yao walikuwa wakisubiri mvolea hiyo ya ruzuku.
Kwa
upande wake katibu wa itikadi na uenezi wa chama cha mapinduzi
(CCM) mkoa wa Njombe Honoratus Mgaya alisema kuwa wananchi hao
wanahoja ya msingi kuhusu viongozi wao ila aliwataka kuondoa hofu
na kuwa Rais anawakilishwa na mkuu wa wilaya kwa upande wa
serikali na upande wa chama mbunge ni mwakilishi wa Rais pia kwa
maana ya mafiga matatu ya CCM kwa maana ya diwani, mbunge na Rais.
Hata
hivyo alisema kuwa iwapo wilaya hiyo ya Ludewa pekee inazaidi
ya vijiji 77 na kata zaidi ya 25 kwa upande wa Tanzania nzima kuna
zaidi ya vijiji vingi zaidi na hivyo wasilalamike kwa Rais kutofika
kata hiyo na kuwa ip siku atafika ama waziri .
Mbunge
wa jimbo hilo la Ludewa Filikunjombe alisema kuwa kwa upande
wake kama mbunge anaendelea kupambana na utatuzi wa kero mbali
mbali zinazowakumba wananchi hao
