CUF WAPINGA ZOEZI LA USAFI MKOANI TANGA LILOPANGWA KUFANYIKA KILA JUMAMOSI

 
Wakati Serikali ikihamasisha usafi wa mazingira katika maeneo yote nchini, Chama cha Wananchi CUF mkoani Tanga kimetoa tamko la kupinga zoezi hilo lililopangwa kufanyika kila Jumamosi kwa madai kwamba wanachama wake watakuwa kwenye shughuli za kimaendeleo. 

Akitoa tamko hilo kwenye mkutano wa hadhara Diwani wa Msambweni, RADHID JUMBE amesema, suala hilo ni la kisiasa na kwamba limepangwa ili kukujenga Chama cha Mapinduzi CCM kisiasa. 

Mkuu wa Mkoa wa Tanga CHIKU GALAWA amewataka wananchi mkoani humo kushiriki zoezi la Usafi kila Jumamosi kufuatia kushuka kwa utekelezaji wa zoezi hilo kama ilivyopangwa hapo awali. 

Hatua hiyo ya Viongozi wa CUF kutangaza mgomo wa kushiriki zoezi la ufanyaji wa usafi katika maeneo yao limedaiwa kuchangiwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga kutowashirikisha madiwani wa chama hicho katika kuutekeleza mpango huo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo